84. Uliyesulibishwa

1 Uliyesulibishwa,
Mtakatifu Bwanangu,
uwe ngao shidani,
uniombee mimi.
Uliyesulibishwa,
Mtakatifu Bwanangu!

2 Wongofu sina hata,
niondolee makosa.
Mwovu akinishtaki,
nasumbuka rohoni.
Wongofu sina hata,
niondolee makosa.

3 Wewe tu nipokee,
nakukimbilia wee.
Hata nifanye bidii,
nikatoe machozi.
Wewe tu nipokee,
nakukimbilia wee.

4 Uwe ngao shidani,
niombee na mimi!
Hapa nikiumizwa,
saa ya mwisho ikija:
Uwe ngao shidani,
niombee na mimi!

Text Information
First Line: Uliyesulibishwa
Language: Swahili
Publication Date: 1988
Topic: Kuteswa na kufa kwa Yesu
Notes: Sauti: "Spanish chant," Brosse Missionsharfe, Erster Band #170, Augustana Hymnal #96
Tune Information
(No tune information)



Suggestions or corrections? Contact us